Tanzania Kukosa Misaada Ya Ulaya

JE, MMEYASIKIA YA BUNGE LA ULAYA.

Bunge la Ulaya limetoa uamuzi mzito unaobeba ujumbe wa kisiasa wa hali ya juu dhidi ya mwelekeo wa utawala wa sasa nchini Tanzania. Kupitia Kamati ya Mambo ya Nje (EP_ForeignAf) na Kamati ya Maendeleo (EP_Development), wabunge wa EU wamepiga kura kuzuia hatua ya Tume ya Ulaya kutoa fedha nyingi kwa Tanzania mwaka ujao kupitia mfuko wa NDICI–Global Europe – mfuko muhimu kwa kukuza maendeleo, ustawi na uwajibikaji barani Afrika.

Katika kura hiyo, wabunge 53 waliunga mkono kusitisha fedha hizo, huku 2 wakipinga na 1 akijizuia kupiga kura. Hii si kura ya kawaida. Ni tamko rasmi la kisiasa la kuonyesha kutoridhishwa na hali ya kisiasa, uchaguzi, na mwenendo wa haki za binadamu nchini.

READ Also  The Wealthiest World Leaders in 2025

Kwa nini wamechukua uamuzi huu?

Sababu zao ni tatu kuu:

  1. Kukithiri kwa ukandamizaji wa wananchi – ikiwemo kubanwa kwa haki ya kujieleza, kuandamana na kukusanyika.
  2. Uchaguzi wenye utata na udanganyifu – kutokuwepo kwa uwazi, haki na uwanja sawa wa kisiasa.
  3. Mwelekeo wa kiimla wa Serikali – kuongezeka kwa matendo yanayoashiria kupotea kwa misingi ya demokrasia.

Kwa lugha nyepesi, Bunge la Ulaya limesema:

“Hatutoendelea kutoa fedha kubwa kwa Tanzania huku demokrasia ikiendelea kupungua na wananchi wakizidi kunyanyaswa.”

Hii ina maana gani kwa Tanzania?

  1. Fedha za maendeleo Zinaweza kuzuia au kucheleweshwa hadi maboresho ya kisiasa yaonekane.
  2. Sifa ya Tanzania kimataifa Inaendelea kuharibika kutokana na tuhuma za ukandamizaji.
  3. Mahusiano ya Tanzania na EU Yanapitia mtihani mkubwa na presha itaongezeka.
  4. Serikali ya Tanzania Itahitaji kuchukua hatua kurejesha imani ya dunia
READ Also  RIP: Sad As Student Allegedly Jump Into Molem Dam

Uamuzi huu unakuja katika kipindi ambacho macho ya dunia yote yapo Tanzania. EU imeonyesha wazi kuwa haitatoa fedha za kujenga barabara na miradi ya maendeleo kwa taifa linaloshutumiwa kubomoa misingi ya haki, uhuru na demokrasia.

Onyo au Fursa?

Serikali inaweza kuchagua:

  1. Ama kuendelea na njia ya sasa na kupoteza washirika muhimu,
  2. Au kuanza kufungua mfumo wa kisiasa na kurejesha matumaini ya wananchi na jumuiya ya kimataifa.

Lakini jambo moja liko wazi:

👉🏽 Dunia imeamka. Na sasa inaangalia Tanzania kwa makini zaidi kuliko hapo awali.

Wasalaam
John Pambalu

  • Related Posts

    UPDATE: China Has Executed 11 Members Of A Criminal Syndicate Convicted Of Luring Foreigners

    China has executed 11 members of a criminal syndicate convicted of luring foreigners — including hundreds of Kenyans — into scam and fraud compounds in northern Myanmar. The group, identified…

    Seé What Sadio Mane Did To The Lady Who Approached Him During AFCON Final

    During the AFCON final, a lady approached Sadio Mané to congratulate him, but she was politely stopped by Mané himself. This action later raised questions, and journalists asked him why…

    You Missed

    UPDATE: China Has Executed 11 Members Of A Criminal Syndicate Convicted Of Luring Foreigners

    • By Milton
    • January 31, 2026
    • 2 views
    UPDATE: China Has Executed 11 Members Of A Criminal Syndicate Convicted Of Luring Foreigners

    Seé What Sadio Mane Did To The Lady Who Approached Him During AFCON Final

    • By Milton
    • January 31, 2026
    • 2 views
    Seé What Sadio Mane Did To The Lady Who Approached Him During AFCON Final

    Gachagua Threatens Nationwide Protests Over Alleged Church Attack

    • By Milton
    • January 31, 2026
    • 3 views
    Gachagua Threatens Nationwide Protests Over Alleged Church Attack

    Xiaomi Launches the REDMI Note 15 Series in Kenya: Titan Durability Meets Pro-Grade Imaging

    • By Milton
    • January 30, 2026
    • 3 views
    Xiaomi Launches the REDMI Note 15 Series in Kenya: Titan Durability Meets Pro-Grade Imaging

    Gachagua Threatens Nationwide Protests Over Alleged Church Attack

    • By Milton
    • January 30, 2026
    • 5 views
    Gachagua Threatens Nationwide Protests Over Alleged Church Attack

    The University Doesn’t Teach You How To Monetize Your Degree

    • By Milton
    • January 30, 2026
    • 5 views
    The University Doesn’t Teach You How To Monetize Your Degree